KATIBU wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Beng’i Issa amewahimiza wafanyabiashara nchini, kujiunga katika vikundi ili kupata sifa za kuzitumia vema fursa katika mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga..
WAFANYABIASHARA nchini wametakiwa kuchangamkia fursa zilizopo katika Mradi wa Bomba la Mafuta ghafi kutoka Kabale Hoima, Uganda hadi Chongoleane Tanga, Tanzania kwa vile asilimia 80 ya bomba hilo litapita nchini.
UTAPIAMLO unaelezwa kuwa ni upungufu wa viini lishe mwilini, na unaelezwa kuwa tatizo la kiafya linaloathiri watoto chini ya miaka mitano, wajawazito, wanaonyonyesha na hata wazee, kutokana na mahitaji ya lishe kuwa makubwa kulinganisha na makundi mengine.
JINA VETA (Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi) ni maarufu miongoni mwa Watanzania wengi kutokana na kuakisi ufundi stadi. Katika makala haya, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dk Bwire Ndazi, anaeleza nafasi ya mamlaka katika kufungua fursa za ajira kwa vijana nchini.
MHARIRI Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Dk Jim Yonazi ametaka wananchi wahabarishwe juu ya fursa zilizopo ili kufikia uchumi wa viwanda.
WATU wengi wanapoanza kufanya biashara wanakuwa hawafanyi utafiti wa kutosha, matokeo yake biashara wanazozianzisha zinakufa. Hivyo basi, biashara unayoifanya ni vema ukazingatia vitu mbalimbali kabla ya kuifungua, ikiwamo eneo la biashara, samani pamoja na muonekano wake kwa wateja wako.
"INAWEZEKANA una sababu za msingi za kuacha biashara uliyoianzisha na kuidumisha kwa kipindi fulani. Kufanya hilo si kosa, ilimradi uamuzi wako usiwe wa kukurupuka, ili usikusukume kujuta baadaye."
Hivyo ndivyo unavyoeleza mtandao wa majibu www.answers.com, ukitoa maelezo mbalimbali kuhusu sababu za msingi zinazoweza kumfanya mfanyabiashara aachane na biashara moja na kuigeukia nyingine, bila kujali kuwa ya awali anayoiacha ilimgharimu muda na fedha nyingi za mtaji.
VIKUNDI zaidi ya 65 vya wajasiriamali wadogo kutoka katika kata zote wilayani Uyui mkoani Tabora, vimewezeshwa mikopo midogo ya zaidi ya Sh milioni 70 katika robo ya kwanza na ya pili ya mwaka wa fedha wa 2016/2017.
SERIKALI imewataka wabunge kuielewa dhana ya ushiriki wa Watanzania katika uwekezaji (Local Content) ili wawe mstari wa mbele kuwaelimisha wananchi kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kiuchumi na uwekezaji nchini.
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, amewataka watendaji wakuu na wafanyakazi wa idara za mikopo za benki, taasisi za fedha na mifuko ya kijamii kote nchini, kuacha kukaa ofisini na badala yake kwenda vijiji kutoa elimu kwa wananchi juu ya fursa za kukopa ili wajiinue kiuchumi.