Kilimo cha Vanila
Mbali na Tanzania, vanilla pia hulimwa katika nchi za Madagascar, Mexico, Uganda, Visiwa vya Comoro na katika visiwa vya Re Union. Hapa nchini zao hili hulimwa zaidi mkoani Kagera lakini sasa limeanza kusambazwa katika mikoa mingine kama vile Morogoro na Kilimanjaro. Hatua hiyo ya kusambaa kwa vanilla imeelezwa kwamba ni kutokana na juhudi za Wizara ya Kilimo na Ushirika.